Desemba 09, 2014

MAJI YA TANGAWIZI NA MDALASINI

015Siku hizi zakaribuni mvua imekua ikinyesha kwa wingi na hali yahewa ni baridi kwa baadhi ya mikoa hapa nchini.Watu hukabiliana na baridi hiyo kwa njia na namna mbalimbali.Hapa jikoni tunakabiliana na baridi kwa kikombe  cha Maji vuguvugu yenye Tangawizi,mdalasini na asali.
Tangawizi na mdalasini vinasifa yakuleta joto mwilini kwa haraka na pia huongeza uwezo wa mwili kumeng’enya na kutumia chakula  (Metabolism).Sifa hizi hufanya viungo hivi kua moja ya viungo muhimu katika kuiweka afya yako salama.Unaweza tumia viungo hivi hata katika mapishi mengine
Mahitaji
  • Maji yamoto kikombe 1
  • Tangawizi kijiko 1 cha chai (inaweza kua yaunga,au sugua tangawizi mbichi kisha kamua maji yake)
  • Mdalasini ½ kijiko chai ( wa unga/uliosagwa)
  • Asali Mbichi  kijiko 1 cha chai
Njia
1.Chemsha maji adi yatokote
2.Katika kikombe weka Tangawizi na mdalasini,kisha mimina maji yamoto.Koroga ili kuchanganya.Funika kikombe kwa dakika tano
  •  Funika kikombe ili kutunza virutubisho na kutunza joto ili liwezeshe uvunaji wa virutubisho kwenye viungo
  • Usichemshe viungo jikoni kwani kufanya hivyo kutapoteza virutubisho na nguvu ya viungo
3.Ongeza asali,koroga .Tayari kwa kunywa.
  • Asali huongezwa baada ya joto la maji kupungua ili kuepuka kuuwa enzymes walio kwenye asali,pamoja na kutunza virutubisho vilivyo kwenye asali
  •  Chuja kabla yakunywa ukipenda
Tafiti za Tiba lishe na virutubisho zinaonyesha kwamba ni lazima kutumia tangawizi kijiko kimoja cha chai Wakati wowote unapotumia tangawizi kama tiba lishe ili kupata matokeo
Naamini kinywaji hiki kitakufaa sana siku za baridi

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni